Maamlaka ya NTSA wiki jana ilichapishwa mswada wa mwongozo unaopendekeza na kutoa kanuni za jinsi magari yote yatakavyokaguliwa ili kudumisha usalama barabarani . Katika mapendekezo hayo ,NTSA itakuwa na maamlaka ya kuwapa ruhusa wafanyibiashara wa kibinafsi kufungua vituo vya kuyakagua magari . Tayari NTSA imeanza kufanya vikao vya umma kuhusu mapendekezo yake .
KMA imesema hatua hiyo ya serikali inalenga kuzidisha ufisadi ambao huambatana na zoezi zima la kuyakagua magari ya usafiri wa umma nay ale ya kibiashara . Murima ,katika taarifa yake ameshangaa jinsi serikali ilivyokosa haya kwa kutaka kutwika mzigo zaidi wenye magari ilhali tozo ya utunzi na ukarabati wa barabara imeongezwa kwa kutoska shilingi 8 hadi shilingi 24 ndani ya kipindi cha miaka miwili .Amesema serikali kwanza inafaa kuziimarisha barabara zote nchini kabla ya kutekeleza pendekezo la ukaguzi wa magari ya kibinafsi .