It was a joke! Willy Paul atoa wimbo na Alaine.

Msanii  Willy Paul maajuzi ameteka mitando ya kijamii akiwataka wakenya kumsaidia afikishe ujumbe wake wa msanii wa Jamaica Alaine ili warudiane kama wapenzi .wengi waliamini kwamba ni ilikuwa ukweli Pozze alikuwa akitaka  uhusiano wa kimapenzi na Alaine .

Lakini imebainika kwamba zote hizo zilikuwa sarakasi za kutaka kuuangazia wimbo wao mpya na Alaine kwa  jina ‘shado Mado’. Wimbo wenye mshiko   mzuri  huenda utatamba endapo  Willy Paul atafaulu kuutangaza vyema mitandaoni na katika mahojiano.

Baada ya wimbo huwekwa youtube mapema  ijumaa ,wengi walionekana kumkashifu Pozze kwa kuwachezea shere kuhusu maandishi yake mtandaoi akidai kwamba Alaine  hakuwa akizungumza naye kwa sababu ya uhusiano wake na staa mwingine za Bongo  Nandy .