Kisa hicho kiliripotiwa kutokea agosti tarehe mbili mwaka huu katika barabara kuu ya Thika karibu na Roysambu baada ya abiria huyo kutofautiana na washukiwa hao wawili . Kimondo aliaga dunia papo hapo baada ya kusukumwa . kondakta wa basi hilo alitorka baada ya tukio hilo lakini basi lenyewe likanaswa na dereva kukamatwa .Baadaye dereva aliachiliwa huru baada ya siku mbili katika hali ya kutatanisha . Ilidaiwa aliachiliwa huru kwa bondi ya polisi yenye thamani ya shilingi elfu 60 pamoja na basi hilo kwa jina zam zam .
OCPD wa Kasarani Peter Kimani alipoulizwa kuhusu kuachiliwa kwa dereva huyo na basi ,alisema liliondolewa hatia . “ Utaratibu wa trfaiki ni kuwa gari linaposababisha ajali ,ukaguzi unafanywa na kisha linaachiliwa .lakini kesi hiyo inaendelea’ amenukuliwa akisema OCPD huyo .