Tazama Chris Osale, Ndugu wa McDonald Mariga anayeng'ara zaidi

72593148_467030287500264_5183629531534820883_n
72593148_467030287500264_5183629531534820883_n
Ndugu wa ukoo wa staa wa soka McDonald Mariga ni kati ya wakenya wanaotia fora zaidi maishani.

Chris Osale ni binamu wake mastaa hawa wawili wa soka (Wanyama na Mariga)

Uraibu wa Chris Osale wa kuvaa nadhifu unamuweka katika nafasi sawa na ndugu zake wanaomiliki utajiri mkubwa.

Victor Wanyama na McDonald Mariga wamepiga hatua kubwa zaidi katika ulingo wa soka.

https://www.instagram.com/p/B39QyUXHHM-/

MacDonald aliamua kustaafu soka na kuzamia siasa.

Uteuzi wa mwanasoka huyu aidha ulikumbwa na dukuduku baada ya bodi ya IEBC kukosa jina lake katika rejista ya wapiga kura.

Staa huyu wa soka hakufa moyo na akazidi kupambana.

Kuna baadhi yao ambao wamenukuliwa kusema kuwa Mariga hawezi kazi ya siasa.

https://www.instagram.com/p/B39QMAiHjVN/

Spika wa kaunti ya Nairobi Beatrice Elachi amenukuliwa na vyombo vya habari akipinga ugombea wa McDonald Mariga.

Elachi ambaye pia ni mwanachama katika mrengo huo wa Jubilee alisema kuwa Mariga hawezi jaza pengo ambalo mwendazake marehemu Ken Okoth aliacha.