"Sio wizi, ni malipo ya Twa twa twa," ajitetea Ruth Khaecha mbele ya korti

Screenshot_from_2019_12_02_12_22_38__1575278582_51322
Screenshot_from_2019_12_02_12_22_38__1575278582_51322
"Sio wizi, ni malipo ya Twa twa twa,"

Haya yalikuwa maneno ya Ruth Khaecha katika mahakama akikana wizi wa kima cha hela Kshs 1,350,000 kutoka kwa mwajiri wake Paul Mwangi.

Ruth ambaye ni kijakazi anashukiwa wizi uliofanyika katika mtaa wa Balozi, Muthaiga.

Mrembo huyu alisema kuwa alilipwa Khs, 800,000 kama zawadi wa Twa twa twa nzuri.

Hakimu Heston Nyaga hata hivyo alimpata Khaecha na makosa ya kuiba kiwango hicho cha hela kutoka kwa bosi wake Mwangi na kumfunga jela miaka 3.

Korti aidha iliagiza sehemu ya ardhi aliyonunua iuzwe ili kuridhia kiasi hicho cha fedha.

Mshukiwa alikuwa amemkabidhi babake Kshs, 500,000 huku 70,000 zikipatikana katika mkoba wake

Khaecha alijitetea kuwa alionyesha tajriba kubwa kitandani ili kupata hela hiyo.

Mrembo aliifungukia mahakama kuwa alianza kufanya kazi Novemba 25 na bosi wake akaanza kumnyemelea kimapenzi.