Aidha, Khaecha alisema kwamba alipewa shilingi 800,000 kama zawadi baada ya kumpa 'mapenzi matamu.'
Hivyo ndivyo alivyotoa ushahidi kortini Januari 15.
Lakini baada ya hakimu Heston Nyaga wa mahakama ya Makadara aliposikiza kesi hiyo tena Ijumaa, Khaecha alipatikana na hatia ya kumuibia mwajiri wake pesa na akahukumiwa kifungo cha miaka 3 gerezani.
Kisha akasema kortini kwamba baada ya kitendo hicho Mwangi alimpa bahasha.
Khaecha aliambia mahakama kuwa aliamua kugura eneo hilo kwa kuwa mkewe, Jane Wairimu alikuwa anashuku kutokana na 'jinsi alivyokuwa akimpigia kelele.'
Aidha alisema kwamba alifanya kazi kwa miezi miwili unusu huku mshahara wake ukiwa shilingi 6,500 kila mwezi.
Mwangi alithibitishia korti kwamba mshtakiwa alilipa hizo pesa na kutoroka bila maagano rasmi.
"Nilipofika nyumbani, nilipata nyumba ikiwa imefungwa, na mshtakiwa hakuwa. Nilijaribu kumpigia simu lakini sikufaulu." alisema