NEW MANDATE:Oparanya Achaguliwa mwenyekiti wa CoG bila kupingwa .

Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya amechaguliwa  bila pingamizi kuwa mwenyekiti wa baraza la magavana . Kupitia mwafaka , magavana  wamewaruhusu Oparanya ,Mwangi wa Iria(Murang’a) na Kivutha Kibwana (Makueni)  kuhudumu kama mwenyekiti ,naibu mwenyekiti na kiranja wa baraza hilo.

Oparanya ambaye ana uhusiano wa karibu wa  kiongozi wa ODM Raila Odinga  ametetea kiti hicho kwa muhula wa pili na wa mwisho .Oparanya  alichukua wadhfa huo  januari mwaka jana kutoka kwa gavana wa Turkana  Josephat Nanok  ambaye aliongoza baraza hilo kwa miaka miwili .

Washililizi wa nafasi hiyo  wameweza kunufaika na  ushawishi mkubwa unaombatana na majukumu yao kwani  mwenyekiti wa CoG  ndiye hutumiwa kama kiunganishi kati ya serikali 47 za kaunti na serikali ya kitaifa .  Oparanya ,Nanok na mwenyekiti wa kwanza Isaac  Rutto aliyekuwa gavana wa Bomet waliweza kupepezwa katika siasa za kitaifa kutoka na wadhfa huo.