Hivi karibuni, mbunge Millie Odhiambo alijipata akipondwa vibaya katika twitter baada ya kuweka ujumbe ulioonekana kuendeleza dhana hii alipoambatisha ujumbe huo wake na picha iliyowalinganisha wanawake wa Kenya na wenzao wa Uganda. Millie alindika hivi ;
‘It is our responsibility as Kenyan women to teach our daughters how to tend to their future husbands. It might appear unfeminine but God has a reason why we are women and they are men... We have to embrace nature and its dynamics’
Wakenya hawakumpa mbunge huyo muda wa kujieleza na pindi makombora ya kumkosoa yakaanza kurushwa. Kwa wakati mmoja, ilibidi Millie afafanue kauli yake kuhusiana na swala hilo lakini alichosema kilizua mengi hasa kuhusiana na mjadala wa chini kwa chini ambao umekuwepo kwa muda mrefu sana kuhusu hadhi, heshima na tabia za wanawake wa Kenya wakilinganishwa na mvuto wa wenzao kutoka Uganda na hata taifa lingine jirani la Tanzania.
https://twitter.com/MabonaMilie/status/1257535478959669248
Ujumbe huo wa mbunge Millie Odhiambo ulizua kumbukumbu ya mhadhiri mmoja wa chuo kikuu jijini Nairobi ambaye alipokonywa mume na mfanyikazi wake, msichana wa Uganda. Wengi hawakuamini kilichofanyika lakini kwa mujibu wa masimulizi ya pande zote husika, msichana huyo kutoka Uganda alimfanya mume wa mhadhiri kujihisi kama mfalme na muda sio mrefu, walikuwa washachukuana na jamaa kumuacha mke wake msomi na mhadhiri wa chuo kikuu!
Yote yalianzia katika vitu ambavyo wanawake wa Kenya husema ni vitu vidogo. Kwa sababu mume wa mhadhiri alikuwa pia msomi, alikuwa mhandisi na mara nyingi akija nyumbani, hakuwa akimpata mke wake akiwa amewasili na nyakati zote, yule mfanyikazi wa nyumbani alikuwa ndiye anamshughulikia kuanzia kumuandalia chakula na hata maji bafuni. Ilifika wakati Engineer akaanza kumpigia simu mfanyikazi wake kumjulia hali kwa sababu mkewe alikuwa kajitosa kweli katika shughuli za taaluma yake na akasahau kabisa jukumu lake lingine kama mke wa mtu .
Muda ulivyodondoka ndivyo Mhandisi alivyojipata kavutiwa kuwa karibu sana na yule mfanyikazi wa kiganda ambaye hakuwa na kisomo wala hungefikiria wangeelewana kwa chochote. Mama mwenye nyumba naye, kwa sababu ya jeuri yake, alikuwa hajawahi kumuona yule mfanyikazi kama tishio kwa ndoa yake kwa sababu alikuwa akijiona kafika kweli kwa sababu ya elimu yake. Kufikia wakati alipofumbua macho kujua kilichokuwa kikiendelea, mfanyikazi wake wa nyumbani, yule mganda alikuwa keshapata mimba ya mumewe na wameanza maisha machoni pake bila haya .