Makachero wa DCI wamtia mbaroni jamaa wa miaka14 kwa kuhusishwa na mauwaji ya mwanahabari.

e0FVjwbU
e0FVjwbU
Maafisa kutoka idara ya ujasusi nchini imemtia kijana wa miaka 14 kwa kuhusishwa na mauwaji ya mwanahabari wa kituo cha Pamoja Fm, Mohammed Marijan Hassan.

Maafisa hao wamesema waliangazia kamera za siri na wako na thibitisho kamili kuwa kijana huyo alihusika katika mauwaji hayo katili ya mwanahabari Marijan.

Marijan aliuwawa yapata wiki moja sasa alipokuwa anatoka kazini mida ya saa 4:00 asubuhi katika mitaa ya Kibra.