Ukaidi wa Tanzania! Wanahabari wa Kenya wapigwa faini ya shilingi 46,000 ama wafungwe jela

EYX29NEWkAULWUV
EYX29NEWkAULWUV
Kufuatia tukio ambapo wanahabari wawili kutoka Kenya walitiwa mbaroni na asasi za usalama wa Tanzania, sasa taarifa zinasema kuwa wanahabari hao Clinton Isimu na mwenzake Kaleria Shadrack wametakiwa kulipa faini ya shilingi 46,000 ama kufungwa gerezani miaka 3.

Wanahabari hao walitiwa mbaroni wakiwa kwa harakati za kutaka kujua hatua ambazo serikali ya taifa  hilo ilikuwa imeweka ili kuzuia maambukizi ya virusi hatari vya corona.