KQ kurejelea kazi hivi karibuni-Uhuru Kenyatta Asema

Kulingana na rais Uhuru Kenyatta kampuni ya ndege za KQ itarejelea kazi hivi karibuni hii ni baada ndege hizo kisitishwa kufanya kazi nchini tofauti kwa sababu ya janga la corona.

KQ imekuwa ikisafirisha mizigo pekee kwa muda wa miezi mitatu, ili kurejesha uchumi wa nchi KQ itaanza kusafirisha abiria humu nchini na hata baadhi ya nchi za nje tofauti.

"Tunafanya kile chote tuwezalo ili kuhakikisha tumerudi angani, tumengoja sana kufungua na tuna hamu ya kufungua lakini lazima tuhakikishe kuwa kila mmoja wetu yupo salama." Uhuru Alisema.

Uhuru alikuwa anazungumza hayo kupitia njia ya video iliyofadhiliwa na ushirika wa Washington.

Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya KQ Allan kilavuka alisema kuwa kampuni imeathirika pakubwa kwa  kupoteza billioni 10, wakati huu wa janga la corona.

Huku KQ ikisafirisha tu mizigo na madawa mapato hayo hayajaweza kifanya biashara kuleta faida wala kuendeleza utumizi wao.