Mabilioni ya Covid 19 yako wapi? Ahoji katibu wa kudumu Macharia aliyepatikana na virusi hivyo

Macharia
Macharia
Katibu wa kudumu aliyepatikana na  covid 19 amehoji  usimamizi wa pesa zinazotolewa kusaidia kupambana na janga la corona  akishangaa zimetumiwa vipi pesa nyingi zizilizotolewa katika hazina ya kupambana na janga hilo.

Katibu wa kudumu wa mashauri ya kigeni Macharia Kamau  alipatikana na virusi hivyo wiki jana  na akumkabidhi  katibu wa diplomasia  balozi  Tom Amollo majukumu yake .

Lakini Macharia alijutia kwamba mpango wa serikaliwa kuwatafuta watu waliotangamana na  waliopatikana na ugonjwa huo umefeli ,hakuna matibabu na utunzi wa walipatikana na ugonjwa huo na pia kampuni za bima zimekataa kugharamia matibabu ya wagonjwa hao .

“ kwa mabilioni yote yaliyotengwa  kw akampeini hii ni jambo la kufadhaisha kwamba hakuna hata mkakati wa kuhakikisha kwamba waliopta ugonjwa huo wanapata  huduma za matibabu au hata kuweza kuwatafuta watu wengine waliotangamana na wagonjwa’ Macharia alisema katika kundi moja la  WhatsApp  la maafisa wakuu wa serikali

Maoni yake hayo huenda  yakalipua kutoridhika kwa namba ambayo wizara ya afya inashughulikia janga hilo  huku pakiwa na hofu kwamba huenda visa vya corona vikalemaza mfumo wa  huduma za matibabu nchini .

Maafisa kadhaa wakuu wa serikali wamekuwa wakipambana pia na virusi hivyo baada ya kuambukizwa wakiwemo mawaziri wawili .

Macharia  amesema pindi tu alipopimwa na kupatikana na virusi vya corona aliwaarifu watu wote aliokutana nao lakini alishangaa kwamba hakuna aliyekua amejulishwa hilo na serikali kumaanisha kwamba mpango huoulifeli kitambo .

Macharia  amesema alikuwa na daalili kama za ugonjwa wa malaria  na kizungungu  lakini bado hajakwnda hospitalini .

NHIF wiki jana ilitangaza kwamba iatagharamia huduma za utunzi kwa wagonjwa wa Covid kwa wagonjwa watakaolazwa katika hospitali zilizoidhinishwa na wizara ya  Afya .