Walimu wa Kiambu washindwa kulipa kodi ,walazimika kuishi madarasani

Muhtasari

 

  •  Walimu hao wanaishi shuleni baada ya kushindwa kulipa kodi 
  • Obuya anaishi katika darasa moja na mkewe na watoto watatu 
  • Walimu wengi wa shule za kibinafsi wameathiriwa na janga la corona baada ya shule kufungwa 
Nguo za walimu nje ya darasa la Shule ya Damacrest

Walimu sita wanaishi na familia zao katika madarasa ya shule katika eneo la Uthiru ,kiambu baada ya kushindwa kulipa kodi za nyumba .

 Walimu hao ni miongoni mwa wengi ambao kipato chao kilikatizwa baada ya shule kufungwa mwezi machi kwa ajili ya janga la corona .

Paul Obuya, 30, ni miongoni mwa walimu ambao wamepewa hifadhi katika shule Damacrest  ambayo ni ya kibinafasi.Obuya  na wenzake watano  ambao hawakutaka kutajwa  anasema walilazimika kuuza  vitu vya nyumba  ili kulipa malimbikizi ya kodi waliokuwa wakidaiwa  kwa sababu hawaku na malipo ya kuendelea kugharamia kodi za nyumba zao .

 Mwezi Aprili mwajiri wao Florence Wamakima aliingilia kati kwa  kuwapa hifadhi kwenye baadhi ya madarasa ya shule yake na hata kuwapa chakula .

 “ Hatuwezi sasa kujilipia kodi ya nyumba na mahitaji mengine ya kimsingi .mkurugenzi wetu alituruhusu kuishi katika mojawapo ya madarasa’ Obuya amesema

 Amesema aliamua kuhamia shuleni humo na mkewe na watoto watatu kwa sababu hakuweza kumudu kodi ya shilingi 7000 kila mwezi .

Walimu wakitoa mafunzo ya mtandaoni kwa wanafunzi

 Nimeuza karibu kila kitu cha nyumba ili kulipa deni la kodi  na nikafaulu kupata shilingi elfu 10 kisha mwenye nyumba  akaniruhusu niondoke’

 Kabla ya janga la corona ,Obuya alikuwa akipokea mshahara wa shilingi elfu 25

 
 

 Walimu hao sasa wamepewa madarasa katika ghorofa ya nne na tano katika jiengo hilo lenye madarasa , afisi ya walimu na  afisi  ya utawala .

 Wakati  mwandishi wa the star alipozuru shule hiyo walimu hao walikuwa wakiwafunza watoto mtandaoni huku familia zao zikiwa darasani .

 Amesema shule huwalipa pesa kiasi za kufanya mafunzo hayo ya mtandao na anatumai mwaka ujao mambo yatakuwa sawa . Mkurugenzi Wamakima anasema wamewapa makao wafanyikazi wengine wasiokuwa walimu . Amesema kabla ya Covid 19 hakupata tatizo la kuwalipa walimu na wafanyikazi wengine lakini kwa sababu wazazi hawalipi karo baada ya shule kufungwa ,hana pesa za kuwalipa .

Wamakima  anasema chaguo lake kuwapa msaada wafanyikazi wake ni kuwapa makaazi ya muda na chakula . Amesema sababu yake kuwasaidia ni kwa ajili mamake naye aliteseka sana wakati akimlea .

 “ Mimi ni hasla  nilizaliwa Kawangware  na kuelewa na mamangu pekee .Tulikuwa watu wa kwanza kuuzwa sukuma wiki karibu na  Nakumatt Prestige  katika baraara ya Ngong .Mamangu hakuweza kumudu  karo ya shule’ Wamakima anasema

Wamakima  anasema baadaye alijiunga na  Precious Blood High School  ambako karo yake Ililipwa na watawa wa kanisa la katoliki .

 Baadaye alikwenda chuo kikuu kwa usaidizi wa HELB  na kuwa mwalimu mkuu katika shule mbali mbali za umma  kati ya mwaka wa 2004 na 2014 kabla ya kuanzisha shule zake .

 “ Najua  umaskini ni nini baada ya kuzaliwa hohe hahe katika eneo la Gatina’ Wamakima amesema

 Amesema walifunza na kuwaajiri watoto kadhaa kama njia moja ya kuirejeshea jamii .

 Shule ya msingi ya  Damacrest Uthiru ina walimu 177 na wanafunzi 800 .shule hiyo iliwahoji na kuwaajiri walimu 26 zaidi kwa matayarisho ya kufunguliwa kwa shule

Walimu wengi nchini hasa wa shule za kibinafasi wamejipata pabaya kwa ajili ya janga la covid 19 baada ya mishahara yao kukatizwa .

Wakamima  anasimamia shule  za  Damacrest za msingi na upili  Thogoto , Dagoretti kusini  katika kaunti ya Kiambu county.