Mwanafunzi apata kichapo cha mbwa kwa kula chapati 5

Muhtasari
  • Maafisa elimu wa eneo hilo wameifunga shule hiyo kwa kutokidhi masharti ya usajili na usafi wa wizara hiyo baada ya kukaguliwa kufuatia tukio hilo
chapati
chapati

Mwanafunzi mmoja anapokea matibabu katika hospitali moja mjini Mombasabaada ya kuchapwa viboko kwa kula chapati tano badala ya ile aliyopewa na shule.

Walimu wameshutumiwa kwa kumpiga mvulana huyo kwa kutumia bomba la kuchota maji lakini uongozi wa shule unasema ni wanafunzi wenzake waliofanyia hivyo.

Mvulana huyo wa miaka 13-ana alama nyeusi mwilini mwake, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani na kanda za video zilizosambazwa mitandaoni.

Wazazi wake wanasema shule haikuwafahamisha kuhusu tukio hilo hadi wiki iliyopita wakati mtoto wao alipozidiwa na ugonjwa.

Madaktari katika hospitali hiyo wanasema mvulana huyo aliumizwa figo vibaya na sehemu zake za siri pia zimejeruhiwa.

Maafisa elimu wa eneo hilo wameifunga shule hiyo kwa kutokidhi masharti ya usajili na usafi wa wizara hiyo baada ya kukaguliwa kufuatia tukio hilo.