- Hata hivyo, aliwaonya viongozi hao kuwa makini na ndege wa mapema ambao wamekuwa wakiunga mkono harakati za Azimio tangu mwanzo
Gavana wa Makueni Kivutha Kibwana amewakaribisha viongozi wa Muungano wa One Kenya kwenye vuguvugu la Azimio La Umoja linaloongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga.
Katika taarifa yake Jumapili, gavana huyo alisema viongozi wa Oka ambao ni Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper na Gideon Moi wa KANU wanaruhusiwa kujiunga na Azimio la Umoja.
Hata hivyo, aliwaonya viongozi hao kuwa makini na ndege wa mapema ambao wamekuwa wakiunga mkono harakati za Azimio tangu mwanzo.
“Kama Mwenyekiti wa Kambi ya Kiuchumi ya Kusini Mashariki (SEKEB), na magavana wenzangu wawili Dkt Alfred Mutua, Charity Kaluki Ngilu na watu wa Ukambani, tunakaribisha OKA ndani ya AZIMIO
Maono makuu ni umoja wa kweli kuokoa na kustawisha Kenya, sio kugawana nyadhifa. Wacha washiriki wapya waheshimu Ndege za Mapema za AZIMIO," alisema.
Ripoti za viongozi wa OKA kutia saini mkataba na Azimio wa Raila zimekuwa nyingi hivi majuzi baada ya kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi pamoja na wa Ford Kenya Moses Wetang'ula kuacha vazi hilo na kujiunga na kambi ya naibu rais William Ruto.
As Chairperson of the South Eastern Economic Bloc (SEKEB), and my two governor colleagues & the Ukambani people, we welcome OKA into AZIMIO. The grand vision is genuine unity to save and prosper Kenya, not to share positions. Let the new entrants honour the Early AZIMIO Birds.
— Kivutha Kibwana (@governorkibwana) February 6, 2022