'Ni mweupe kama theluji,'Wakili wake pasta Ezekiel asema

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Rhodah Onyancha alisema kuna madai ya vifo vilivyoripotiwa katika eneo lake.

Muhtasari
  • Akizungumza siku ya Alhamisi, wakili huyo alisema hajui kama Mchungaji Paul Mackenzie wa Good News International Church ana uhusiano wa karibu na Ezekiel.
Pasta Ezekiel akamatwa, mbunge wa Magarini amtetea vikali.
Pasta Ezekiel akamatwa, mbunge wa Magarini amtetea vikali.
Image: Twitter

Wakili wa mwinjilisti Ezekiel Odour, Jared Magolo, amesema polisi hawatapata chochote kuhusu mchungaji huyo.

Akizungumza siku ya Alhamisi, wakili huyo alisema hajui kama Mchungaji Paul Mackenzie wa Good News International Church ana uhusiano wa karibu na Ezekiel.

“Tumezungumza na maafisa hao na wanaendelea na uchunguzi watatujulisha kinachoendelea,” alisema.

Alisema mchungaji huyo atatambuliwa na polisi mara watakapomaliza kumhoji.

Wakili huyo alipoulizwa iwapo anajua alipo mke wa mchungaji Ezekiel, alisema hajui kuwa ana mke.

Haya yanajiri baada ya kasisi Ezekiel wa New Life Prayer Centre and Church kukamatwa Alhamisi asubuhi.

Kasisi huyo, mnamo Jumatano, alihojiwa kwa saa nyingi kwa madai kuwa kanisa lake linajihusisha na uchawi.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Rhodah Onyancha alisema kuna madai ya vifo vilivyoripotiwa katika eneo lake.

Polisi walisema hatua ya kumwita Jumatano ilichochewa na uchimbaji wa miili unaoendelea kutoka shambani katika Msitu wa Shakahola.