Maliha kuivunja rekodi ya dunia ya kupika kw muda mrefu zaidi

Mpishi huyo anayeishi Mombasa amewai kuvunja rekodi hio ya Guinness Book of World mara mbili.

Muhtasari

• Alichapisha video katika akaunti yake ya Instagram kutangaza juhudi zake za kuvunja rekodi hio, Chef Maliha alisema amekuwa akifanya mazoezi kwa bidii.

• Maliha anasema atafanya majaribio ya kupika Mei 26 huku akitarajia kupika rasmi mwezi Agosti.

Mpishi mkenya Maliha Mohammed
Mpishi mkenya Maliha Mohammed
Image: INSTAGRAM

Mpishi wa Kenya Maliha Mohammed anapania kuivunja rekodi ya dunia baada ya mpishi wa Nigeria Hilda Baci kuweka rekodi ya kutumia muda mwingi kupika.

Mpishi huyo anayeishi Mombasa amewai kuvunja rekodi hio ya Guinness Book of Records mara mbili.

Alichapisha video katika akaunti yake ya Instagram kutangaza juhudi zake za kuvunja rekodi hio, Chef Maliha alisema amekuwa akifanya mazoezi kwa bidii ili kumwezesha kuvunja rekodi hio.

"Najua watu wamekuwa wakijiuliza chef Maliha amekuwa akifanya nini, anafanya nini, hatujamsikia kwa muda mrefu, niko hapa, niko kwenye mazoezi sasa hivi," alisema.

Maliha anasema atafanya majaribio ya kupika Mei 26 huku akitarajia kupika rasmi mwezi Agosti.

"Mwaka wa 2019, nilivunja Rekodi ya Dunia ya Guinness, kwa kupika saa 7, mwaka wa 2018 nilifanya vivyo hivyo kwa kupika saa 72." Maliha aliongeza.

“Mwaka 2023 bila shaka nilikuwa tayari nimepanga, nilituma maombi yangu mara ya mwisho Desemba 2022, inawachukua muda kukubali maombi yako, walikubali maombi yangu kwa njia ya barua pepe, bila shaka safari hii sitavunja. rekodi moja, lakini mbili."

Atakuwa akipika mbele ya kamera za moja kwa moja nyumbani kwake Tudor huko Mombasa.

"Rekodi ya kwanza itavunjwa Inshallah mnamo Agosti 11, na jaribio la pili la kuvunja rekodi itakuwa Novemba 2023."