Utata

Mahakama kuu yafutilia mbali miswada 23 iliyopitishwa na bunge la kitaifa

Senate yapata afueni baada ya bunge kustwa na mahakama

Muhtasari

 

  •  Maseneta wamekuwa wakilalama kuhusu kupuuzwa na wabunge 
  • mzozo huo ulionekana mwanzoni kama mapigano ya maamlaka 
Spika wa bunge Justin Muturi na mwenzake wa Senate Ken Lusaka

 

Mahakama kuu imefutilia mbali miswada 23 iliyopitishwa na bunge bila kulihusisha bunge la senate .

 Jopo la majaji watatu siku ya alhamisi limeamuru kwamba  spika wa bunge anafaa kumhusisha mwenzake wa senate .

  “ sheria  hizo tata zinakiuka  vipengee vya 96,109,110,111,112 na 113 vya katiba  na hivyo ni ukiukaji wa katiba’Majaji hao wameamuru .

 Baadhi ya  miswada  ambayo  imeathiriwa ni ule wa kompyuta na kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni na ule wa Fedha wa mwaka wa 2018 .

 Katika kesi hiyo senate ilikuwa imewasilisha  kesi  kortini  kupinga uamuzi wa  wa bunge kupitisha miswada hiyo  bila mchango wa  maseneta .

 kuhusu gharama ya kuifutilia mbali miswada hiyo majaji wamesema bunge lingefikiria kwanza kuhusu kupitisha misawada hiyo bila mchango wa senate .

 bunge la kitaifa lilikuwa limesema kwamba kuifutilia mbali misawada hiyo  ni hatua itakayosababisha hasara kubwa kwa serikali  kwa sababu ya gharama yake .

 Mahakama  pia imesema  kwamba marekebisho ya  sehemu ya 4 ya sheria kuhusu ununuzi wa bidhaa za matibabu  ni ukiukaji wa sheria  na hivyo basi kinyume cha katiba .

  Maseeta wamekuwa katika mzozo wa muda mrefu na  bunge kuhusu wajibu wao katika  masuala ya utayarishaji wa sheria .

 Wamekuwa wakiwashtumu wenzao wa bunge la kitaifa  kwa kuwapuuza na kuhujumu majukumu yao . bunge kwa upande wake  limedai kwamba maseneta wanataka kujipa majukumu yasio yao  kwa kufanya kazi sawia ni ile ya wabunge