- Uteuzi wake uliidhinishwa na bunge wiki jana
- Kassait anakuwa mtu wa kwanza kuishikilia nafasi hiyo
- Awali alikuwa akifanya kazi katika tume ya IEBC
Immaculate Kassait ameapishwa kuhudumu kama kamishna wa data baada ya rais kuweka uteuzi wake katika gazeti rasmi la serikali .
Kassait alikula kiapo siku ya jumatatu katika afisi ya msajili mkuu kwenye hafla iliyoongozwa na msajili wa mahakama ya juu zaidi Moses Serem .
Kiapo hicho kilisimamiwa na afisa kutoka afisi ya msajili mkuu wa idara ya mahakama Sharon Mwayuli.
Kassait atahudumu katika wadhifa huo mpya kwa muda wa miaka 6 baada ya kamati ya bunge kuhusu ICT kuidhinisha uteuzi wake . Awali kabla ya kuteuliwa katika nafasi hiyo Kassait alikuwa mkurugenzi wa IEBC kuhusu usajili wa wapiga kura .
Kamishna huyo wa data pia amewahi kufanya kazi katika taasisi ya elimu na demokrasia na kama afisa wa mipango katika shirika la FIDA Kenya