Muhtasari
- IEBC imeidhinisha muundo wa ukusanyaji wa saini
- zoezi hilo litazinduliwa siku ya jumatano
Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imetoa muundo wa jinsi sahihi za BBI zitakavyokusanya kuanzia hapo kesho wakati zoezi hilo litakapozinduliwa
Katika barua kwa kamati inayoongoza shughuli hiyo mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati amesema wameidhinisha muundo utakaotumiwa wakati wa ukusanyaji wa sahihi hizo ili kurekebisha katiba kupitia kura ya maoni .
Barua hiyo ilikuwa majibu ya barua iliyokua imeandikwa na kamati hiyo ikitaka idhini ya muundao unaofa kutumiwa .
Kamati ya usimamizi wa mchakato wa BBI imesema kwamba inalenga kukusanya sahihi milioni katika kipindi cha wiki moja . zoezi hilo litafanyika kesho baada ya kuahirishwa wiki jana .