Kinoti akana madai

Kinoti sasa akanusha kwamba DCI inalenga kuzifufua kesi za PEV

Kuna hofu kutoka kwa washirika wa DP Ruto kuhusu uamuzi huo

Muhtasari
  •  Kinoti amesema hakuna mpango wa kuzifufua kesi hizo 
  •  Jana waathiriwa wa ghasia za 2007/08 walifurika makao makuu ya DCI kuandikisha taarifa 

 

Mkuu wa DCI George Kinoti

 Mkurugenzi mkuu wa DCI George Kinoti amekanusha madai kwamba idara yake inalenga kuzifufua kesi za ghasia za uchaguzi za mwaka wa 2007/08  .

Kinoti  siku ya jumanne amesema kikao chake siku ya jumatatu na wanahabari hakikulenga  kumaanisha kwamba DCI ilikuwa ikizifufua kesi za ghasia za baada ya uchaguzi .

 Amesema hatua hiyo ilitokana na  na hofu kutoka kwa baadhi ya wakenya ambao walitaka kuhakikishiwa na DCI kwamba hapatatokea tena ghasia za uchaguzi  na  kwamba idara ya DCI itachunguza kesi zote za vitishoi dhidi ya wakenya .

 Amesema wamepokea ripoti nyingi kuhusu wananchi ambao wanahofishwa na uwezekano wa kupoteza mali yao na kaisha yao kwa ajili ya vitisho wanavyopokea .

 Ilikuwa imeripotiwa kwamba serikali imegeuza nia na sasa inataka kuzifufua tena kesi za ghaia za baada ya uchaguzi huo  ikiwemo kisa cha mauaji ya watu katika kanisa la Kiambaa .

 Hatua hiyo imejiri miaka saba baada ya serikali kufunga kesi hizo ikisema  hakuna ushahidi  wa kuwafungulia mashtaka waliotekeleza ghasia ,mauaji na uharibifu wa mali  baada ya watu 1300 kufariki na Zaidi ya 650,000 kutoroka makwao .

 Wiki tatu zilizopita  wakili wa waathiriwa Paul Gicheru alijisalimisha kwa mahakama ya ICC hatua ambayo ilizua tumbo joto katika kambi ya naibu wa rais William Ruto na washirika wake wamedai kwamba hatua ya DCI ni muendelezo wa hila dhidi yake kumzuia kuchukua usukani wa serikali mwaka wa 2022 .

Kinoti  baada ya kukutana na waathiria wa ghasia hizo waliofurika DCI kuandikisha taarifa alisema wamepokea ripoti 72 z amauji na 44 za mizozo ya mashamba huku  kesi 118 za vitisho zikisajiliwa kuhusiana na ghasia za 2007/2008