- Takwimu za NACC zaonyesha kwamba visa 41,728 vipya vya maambukizi vilisajiliwa mwaka huu huku visa 25,062 vikiwa vya wasichana ilhali wavulana ni 16,666
- Data zaonyesha kwamba visa vipya vya maambukizi 6,247 ni vya watoto walio na kati ya umri wa miaka 15-19 . kati ya visa hivyo 4,254 ni wasichana ilhali 993 ni wavulana
Watoto wa shule wanasheni sehemu kubwa ya maambukizi mapya ya HIV kulingana na takwimu za baraza la kupambana na HIV NACC . Wasichana wado ndio waathiriwa wakubwa wa ugonjwa huo .
Takwimu hizo zimeonyesha kwamba mwaka huu pekee visa vipya 21,404 vya maambukizi ni vya watoto wanaoenda shule . Idadi hiyo ni Zaidi ya jumla ya maambukizi ya HIV yaliosajiliwa kote nchini mwaka jana .
Takwimu za NACC zaonyesha kwamba visa 41,728 vipya vya maambukizi vilisajiliwa mwaka huu huku visa 25,062 vikiwa vya wasichana ilhali wavulana ni 16,666
Wale walio na umri wa miaka 15 na Zaidi ni 34,610 ilhali visa 6,806 ni vya wanafunzi walio na umri wa miaka 14 na chini .
Kisumu, Nairobi, Siaya, Homa Bay, Migori, Nakuru, Mombasa, Kisii, Kakamega na Kiambu ni kaunnti zinazoshikilia kumi bora kwa idadi ya juu ya maambukizi mapya mwaka huu
Data zaonyesha kwamba visa vipya vya maambukizi 6,247 ni vya watoto walio na kati ya umri wa miaka 15-19 . kati ya visa hivyo 4,254 ni wasichana ilhali 993 ni wavulana .
Kitengo hicho kinasheheni wanafunzi wa shule za msingi na Upili .
Kwa mujibu wa takwimu hzo visa vingIne vipya vya maambukizi 8.191 vilisajiliwa miongoni mwa walio na umri wa miaka kati ya 20-24 . kati yao 5,166 ni wasichana ilhali 3,014 ni wavulana katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu