Siasa

Uhuru anatumia BBI kusalia madarakani-Mbunge Alice Wahome

meongeza ; ‘Hafai kuruhusiwa kuongeza muda wake madarakai kwa njia moja au nyingine’

Muhtasari
  • Wahome  kupitia taarifa amesema BBI  ni njama  inayolenga kumweka Uhuru madarakai hata wakati kipini chake afisini kitakapokamilika mwaka wa 2022 .
  •   Amewaonya wakenya kwamba watajutia Iwapo marakebisho ya katiba yanayopendekezwa na Uhuru na kiongozi wa ODM Raila Odinga yatapitishwa .
Mbunge wa Kandara Alice Wahome

Mbunge wa kandara Alice Wahome  kwa mara nyingine tena amemshambulia rais Uhuru Kenyatta kwa kutumia BBI kama njia ya kusalia madarakani baada ya muhula wake wa pili kutamatika .

 Mbunge huyo siku ya jumamosi  alidai kwamba  rais analenga kurekebisha katiba ya mwaka wa 2010  ili kumsaidia  kuthibiti  madaraka ya serikali  akiwa nje ya uongozi .

Wahome  kupitia taarifa amesema BBI  ni njama  inayolenga kumweka Uhuru madarakai hata wakati kipini chake afisini kitakapokamilika mwaka wa 2022 .

  Amewaonya wakenya kwamba watajutia Iwapo marakebisho ya katiba yanayopendekezwa na Uhuru na kiongozi wa ODM Raila Odinga yatapitishwa .

 “ Kwa Kenya kusalia nchi ya  demokrasia ya kweli rais wetu anafaa kukubali kwamba hatamu yake inafika tamati .Anafaa  kuhakikisha kwamba madaraka yanakabidhiwa mtu mwingine kwa njia  ya Amani na aende nyumbani’ amesema Wahome .

 Ameongeza ; ‘Hafai kuruhusiwa kuongeza muda wake madarakai kwa njia moja au nyingine’

 Sio mara ya kwanza kwa Wahome kumshtumu rais Uhuru kwa kuwa na lengo la kusalia madarakani baada ya kutamatika kwa kipindi chake mwaka ujao .

 Wahome, ambaye ni  mshirika wa karibu wa naibu wa rais William Ruto  pia amemtaja Uhuru kama tishio kubwa kwa demokrasia ya kikatiba  ,ugatuzi  na rais aliyesimamia kuvurugwa kwa uchumi wan chi katika miaka  yake mitano uongozini .