- Msemaji wa Gideon amethibitisha kwamba kiongozi huyo wa KANU alikuwa katika eneo hilo baada y kualikwa na wazee wakiongozwa na Christopher Koyogi .
- Wazee hao mwaka jana walikutana na naibu wa rais William Ruto na kumbpa Baraka kama msemaji na kiongozi wa jamii ya wakalenjin .
Seneta wa Baringo Gideon Moi siku ya jumamosi alikutana na kundi la vijana waliozuia kundi lake njiani kwenda katika mkutano wa alfajiri na wazee wa ukoo wa Talai huko Nndi .
Wazee hao mwaka jana walikutana na naibu w arais William Ruto na kumbpa Baraka kama msemaji na kiongozi wa jamii ya wakalenjin .
Mamia ya vijana waliziba barabara zinazoelekea Kapsisiywa ambako Gideon alikuwa amewaalika baadhi ya wazee kwa hafla ya kumpa pia Baraka huku uhsama wa kisiaa kati yake na naibu wa rais William Ruto ukizidi tunapolekewa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka wa ujao .
Gideon na kundi lake waliwasili katika eneo holo mwendo wa saa kumi alfajiri katika msafara wa magari Zaidi ya manne na ni katika barabara ya Sangalo-kabiyet ambako msafara wao ulizuiwa na vijana walioiziba barabara kwamba tayari wazee wa Talai walikuwa wameshampa Ruto Baraka za kuwa kiongozi wa jamii hiyo
Msemaji wa Gideon amethibitisha kwamba kiongozi huyo wa KANU alikuwa katika eneo hilo baada y kualikwa na wazee wakiongozwa na Christopher Koyogi .
Gideon alilazimika kuwashawishi vijana hao kukoma kuzua rabha kwani alikuwa na haki kama mkenya yeyote kuzuru eneo hilo .Baadaye alikutana na wazee hao lakini haijafahamika Iwapo sherehe hiyo ya kumpa Baraka itafanyika .