Muhtasari
- Waliuvunja mlango na kuingia ndani lakini wakati huo mzee huyo alikuwa ameshachomeka
- Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo
Mwanamume mmoja ameteketea hadi kufa katika nyumba yake kijijini Nyankoba huko Nyamira .
Kulingana na naibu wa chifu wa eneo hilo Eric Marando, Harrison Morori mwenye umri wa miaka 70 alichomeka akiwa nyumbani kwake alikoishi peke yake.
" Iliripotiwa kwamba moto ulianzia katika sebule yake ambapo majirani walikimbia kumuokoa lakini hawakufaulu’ amesema naibu huyo wa chifu .
Ameongeza kwamba wanakijiji walijaribu kuingia katika nyumba hiyo lakini wakagundua kwamba mlango ulikuwa umefungiwa ndani. Waliuvunja mlango na kuingia ndani lakini wakati huo mzee huyo alikuwa ameshachomeka. Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo