Shule

Wanafunzi hawatakubaliwa kuwa na sanitizer shuleni-Magoha

Magoha amesema ni lita tano pekee za sanitizer zitakazokubaliwa shuleni na zitahifadhiwa na walimu

Muhtasari
  • Alisema kemikali hiyo ina asilimia 70 ya pombe na inaweza kutumia vibaya na wanafunzi .
  •  “ watoto wetu wana ubunifu sana na tunajua  wanachoweza kufanya kutumia sanitizer . hatutaruhusu Zaidi ya litano tano za sanitizer katika  kila shule’ amesema  Magoha .
waziri wa Eimu George Magoha

 Serikali haitaruhusu shule kuwa na kiasi kikubwa cha  sanitizer shuleni ,waziri wa elimu George Magoha amesema .

 Magoha amesema ni lita tano pekee za  sanitizer zitakazokubaliwa shuleni  na zitahifadhiwa na walimu . Alizungumza hayo katika shule ya msingi ya  Kiangochi  siku ya jumamosi akifnya ukaguzi wa matayarisho ya kufunguliwa kwa shule   . Alisema kemikali hiyo ina asilimia 70 ya pombe na inaweza kutumia vibaya na wanafunzi .

 “ watoto wetu wana ubunifu sana na tunajua  wanachoweza kufanya kutumia sanitizer . hatutaruhusu Zaidi ya litano tano za sanitizer katika  kila shule’ amesema  Magoha .

 Pia aliongeza kwamba Zaidi ya maski milioni 7 zimetolewa kusambazwa kwa wanafunzi maskini kote nchini .