- Duru zaarifu kwamba jaji wa mahakama ya juu Zaidi Mohamed Ibrahim anatarajiwa kuchukua usukani kama kaimu jai mkuu .
- Mwilu ambaye ndiye kaimu rais wa mahakama ya juu Zaidi alionekana kuwa kifua mbele katika kinyang’anyiro cha kumrithi Maraga .
Kaimu jaji mkuu Philomena Mwilu amepata pigo katika azma yake ya kutaka kumrithi mtangulizi wake David Maraga . katika hatua moja mahakama kuu imefanya maamuzi manne ambayo yanatia hatarini uwezo wa Mwilu kuichukua nafasi hiyo kwa njia ya kudumu .
Mahakama kuu imetoa uamuzi wa kumuondoa Mwilu katika nafasi yake kama naibu jaji mkuu ,mwanachama wa tume ya JSC ,Jaji wa mahakama ya juu Zaidi na msimamizi mkuu wa kuafikia haki katika idara ya mahakama .
Hatua hiyo pia inamaanisha kwamba Mwilu atakoma kuhudumu kama kaimu wa jaji mkuu na mwneyekiti wa tume ya JSC nafasi ambazo ni muhimu alizochukua baada ya kustaafu kwa Maraga .
Jaji Patrick Jeremy Otieno ndiye aliyetoa uamuzi huo siku ya ijumaa na sasa hatua hiyo inamzuia Mwilu dhidi ya kuongoza vikao vya JSC na hivyo basi kumbandua kutoka mchakato mzima wa kumtafuta jaji mkuu mpya .
Duru zaarifu kwamba jaji wa mahakama ya juu Zaidi Mohamed Ibrahim anatarajiwa kuchukua usukani kama kaimu jai mkuu .
Mwilu ambaye ndiye kaimu rais wa mahakama ya juu Zaidi alionekana kuwa kifua mbele katika kinyang’anyiro cha kumrithi Maraga .
Uamuzi huo wa mahakama ulitolewa Meru baada ya Isaiah Mbiti kuwasilisha kesi kupinga kuwepo kwa Mwilu afisini kwa madai ya kutumia vibaya maamlaka ya afisi yake
Mbiti alidai kwamba kuendelea kusalia kwa Mwili afisini huku akikabiliwa an kesi ya ufisadi ni mapendeleo na ukiukaji wa suta ya sita a katiba .