Serikali yatoa ksh30.5b kwa shule, mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu

Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 30.5 kugharamia elimu ya shule za upili, na mikopo ya ufadhili wa masomo kwa wanafunzi katika vyuo vikuu.

Muhtasari

• Pesa hizo zitapokelewa shuleni kabla ya kufungwa kwa Likizo ya Aprili wiki ijayo.

• Shilingi bilioni 16 zikigharamia ruzuku ya wanafunzi chini ya mpango wa elimu ya bure katika Shule za Sekondari.

wanafunzi wa Roma school Uthiru picha Roma school Uthiru /facebook
wanafunzi wa Roma school Uthiru picha Roma school Uthiru /facebook

Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 30.5 kugharamia elimu ya shule za upili, na mikopo ya ufadhili wa masomo kwa wanafunzi katika vyuo vikuu.

Kwa pesa hizo shilingi bilioni 7 zitagharamia shule za umma katika kiwango cha Junior Secondary huku bilioni 16 Bilioni zikigharamia ruzuku ya wanafunzi chini ya mpango wa elimu ya bure katika Shule za Sekondari.

Pesa hizo zitapokelewa shuleni kabla ya kufungwa kwa Likizo ya Aprili wiki ijayo. Katika ngazi ya elimu ya juu, Serikali imetoa Shilingi bilioni 6.794 kwa ajili ya mikopo kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELB) huku shilingi bilioni 3.98 zikitolewa kwa ufadhili wa masomo kupitia Hazina ya Vyuo Vikuu (UF). Hii inafikisha shilingi bilioni 32 na bilioni 12 Bilioni, jumla ya kiasi kilichotolewa na Serikali kwa mikopo na ufadhili wa masomo mtawalia mwaka huu wa kifedha.

Mwezi Januari mwaka huu, Serikali ilitoa shilingi bilioni l14.4 kugharamia ufadhili wa masomo na mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika vyuo vikuu wanaofadhiliwa na Serikali chini ya Mtindo Mpya wa Ufadhili wa Elimu ya Juu. Mikopo hiyo pia ilihusu mikopo ya muhula wa pili wa Mwaka wa Masomo wa 2023/2024 kwa wanafunzi wanaoendelea.

Mnamo Oktoba mwaka jana, Serikali ilitoa Ksh5.3 Bilioni kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi na Ksh3.9 Bilioni zaidi kwa ajili ya ufadhili wa masomo kwa miaka ya kwanza chini ya Mfumo Mpya wa Ufadhili na Ksh10.3 Bilioni zilitolewa kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELB) mwezi Septemba 2023 kufadhili wanafunzi wanaoendelea na mikopo katika Vyuo Vikuu na Vyuo vya TVET.

Wanafunzi waliofanya Mtihani wa KCSE mwaka wa 2023 watakuwa kundi la pili la wanafunzi kufadhiliwa chini ya mfumo mpya wa ufadhili watakapojiunga na vyuo vikuu na Vyuo vya anuai mwaka huu.