Mke wa aliyekuwa gavana Mwangi Wa Iria, kaka yake wakamatwa kwa ubadhirifu wa Ksh.140M

EACC inawasaka washukiwa wengine sita, akiwemo Gavana wa zamani

Muhtasari
  • Msemaji wa EACC Eric Ngumbi alisema wawili hao walikamatwa Jumatano na kusindikizwa hadi katika Mahakama ya Kupambana na Ufisadi Milimani ili kufikishwa mahakamani.
Image: EACC/ X

Mke wa aliyekuwa Gavana wa Murang’a Mwangi wa Iria, Jane Waigwe Kimani na kakake Solomon Mutura Kimani wamekamatwa kwa madai ya ufisadi.

Wawili hao ni washukiwa wa kesi ya ufisadi ya Ksh.140 milioni Kaunti ya Murang’a.

Msemaji wa EACC Eric Ngumbi alisema wawili hao walikamatwa Jumatano na kusindikizwa hadi katika Mahakama ya Kupambana na Ufisadi Milimani ili kufikishwa mahakamani.

Wawili hao ni Wakurugenzi wa Kampuni ya Value View Ltd, moja ya kampuni zinazosemekana kutumika kama njia ya kupitishia mpango huo wa ulaghai.

EACC inawasaka washukiwa wengine sita, akiwemo Gavana wa zamani, ambaye alikosa kuheshimu wito wa kufika mbele ya EACC Jumatano asubuhi.