Hassan Oktay ajiweka mbali na madai yake Manishinmwe

Mkufunzi wa klabu ya Gor Mahia, Hassan Oktay amekanusha madai kuwa klabu hio imemsajili kiungo wa Rwanda Djabel Imanishinmwe. Hassan ameleza kuwa hajapeana maagizo yoyote kuwa anahitaji kiungo huyo mshambulizi kwa viongozi wa klabu ya Ko'galo.

"Mimi simjui kijana mwenyewe na wala sijasema niletewa yeye kwa timu yangu kwani. Tena, nilipoteza mshambulizi wala sio kiungo hivyo basi nahitaji mshambulizi kulijaza pengo aliloacha Tuyisenge," Hassan alisema.

Mshambulizi wa Bourmouth Callum Wilson ametia sahihi mkataba mpya na club hio. Wilson alifunga magoli 15 na kupika mengine 10 kwa mechi 33 alizocheza msimu uliopita. Klabu ya Chelsea ilikuwa karibu kupata sahihi ya mshambulizi huyu ila ikahamia kwake Gonzalo Higuain wa Juventus.