"Joe Kadenge alikuwa kielelezo muhimu sana cha ubora wa kandanda ya Kenya .Ni huzuni kwamba mkono wa kifo umetupokonya mtu aliyejitolea kuiletea Kenya fahari na taadhima wakati wake’ Rais amesema .Kadenge, amekuwa akiugua kwa muda mrefu na ametajwa kama mshambulaiji bora wa sokamabaye Kenya imewahi kuwa naye . msemo maarufu wa 'Kadenge na mpira' ulitokana na umahiri wake alipokuwa akisakata soka ,na watangazaji wengi wa mpira walikuwa wakisisimka sana wakati marehemu Kadenge alipokuwa na mpira uwanjani .
Miaka miwili iliyopita , Rais Kenyatta na Mama wa taifa Margaret Kenyatta walimtembelea Kadenge aliyekuwa nyumbani kwake mtaani Mariakani jijini Nairobi ili kumtakia nafuu .‘Joe alikuwa rafiki wangu ,alikuwa na maneno ya busara alioniambia wakati mimi na mama wa taifa Margaret tulipomtemebelea’ amekumbuka Rais .Joe Kadenge alikuwa mwanasoka mahiri sana siku zake na aliichezea timu ya taifa Harambee stars kwa miaka 14 baada ya kuanza kusakata boli miaka ya sitini . Baada ya kustaafu kutoka soka ,Joe alijitosa katika usimamizi wa kandanda ambapo pia alipaa na kuwa kocha wa timu ya Haramve Stars mwaka wa 2002. Mwenyezi mungu na aijalie nafsi yake na kuipa ujasiri familia na rafiki zake .