Man United waandikishwa ushindi wao mkubwa zaidi tangu Agosti

greenwood
greenwood
Meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anasema kikosi chake kilikua na mpango wa jinsi wangecheza msimu huu waliwapowanyuka Partizan Belgrade na kufuzu kwa 32 bora katika ligi ya Uropa.

Mabao ya kipindi cha kwanza ya Mason Greenwood na Anthony Martial yalifuatiwa na la Marcus Rashford baada ya mapumziko na kutamatisha ushindi mkubwa zaidi wa United tangu Agosti. Ushindi huo unakiweka kikosi cha Solskjaer kileleni mwa kundi L.

Aaron Ramsey amekiri kua alimwomba radhi Cristiano Ronaldo kwa kukatiza na kumnyima rekodi nyingine ya ligi ya mabingwa.

Raia huyo wa Wales aliwaweka waItalia mbele baada ya dakika tatu tu za mechi yao waliowanyuka Lokomotiv Moscow 2-1 jumatano baada ya kuzuia mkwaju wa adhabu wa Ronaldo.

Katika mchakato huo Ramsey alimnyima mreno huyo rekodi ya Champions League ya kufunga dhidi ya vilabu vingi zaidi lakini akakiri kuwa hisia zake ziliingilia kati ili kuhakikisha timu yake inafunga.

Mabao mawili ya kipindi cha pili yaliwapa Rangers ushindi dhidi ya Porto na kukaribia kufuzu kwa awamu ya mchujo ya mishuano ya ligi ya Uropa.

Vijana wa Steven Gerrard Alfredo Morelos na Steven Davis walifunga mabao ya Rangers. Matokeo haya yana maana kuwa Rangers wako kileleni mwa kundi G pamoja na Young Boys wa Uswizi wakiwa na mechi mbili zilizosalia, huku Porto na Feyenoord wakiwa alama tatu nyuma.

Kocha wa Harambee Starlets David Ouma ametoa wito kwa wakenya kujitokeza kuwashabikia kinadada hao katika mechi yao ya kufuzu kwa michuano ya Olimpiki dhidi ya Shepolopolo ya Zambia hii leo ugani Kasarani.

Hakuna ada ya kiingilio ya mchuano huo kwani FKF inataka mashabiki wengi zaidi kujitokeza kuwashabikia Starlets. Mechi ya marudio itachezwa Lusaka siku ya Jumatatu.

Arsene Wenger amekanusha fununu kuwa anajadiliana na Bayern Munich kuwa meneja wao mpya lakini amejiepusha kujiondoa kutoka kwa kinyang'anyiro hicho. Miamba hao wa Ujerumani wanamtafuta meneja mpya baada ya kumfuta kazi Niko Kovac, baada ya kunyukwa mabao 5-1 na Eintracht Frankfurt.

Wenger alishinda ligi ya Primia mara tatu na kombe la FA Cup mara saba katika tajriba yake ya miaka 22 North London kabla ya kuondoka mwaka wa 2017-18.