Mbwana Samatta afurahia kutimiza ndoto za mashabiki wa Tanzania

samatta
samatta
Mbwana Samatta anasema anafurahia kutimiza ndoto ya mashabiki wa soka wa Tanzanian ya kumuona mmoja wao akicheza katika ligi ya Uingereza. Samatta aliweka historia jumamosi kwa kuwa si tu mtanzania wa kwanza kucheza katika ligi ya Primia bali pia wa kwanza kufunga bao. Mchezaji huyo wa umri wa miaka 27 alifunga bao moja Aston Villa walipopoteza 2-1 kwa Bournemouth. Mashabiki wengi wa soka nchini Tanzania walikusanyika katika mikahawa kumtazama akicheza. Samatta amesema amepokelewa vyema kwenye timu hio haswa wachezaji wa asili ya kiafrika.

https://radiojambo.co.ke/picha-ya-siku-maelfu-ya-watanzania-wajitokeza-kutizama-mbwana-samatta/

Shirikisho la soka nchini  FKF jana lilizindua bodi itakayosimamia uchaguzi utakaofanyika Machi tarehe 30. Bodi hilo itaongozwa na Kentice Tikolo, Patrick Onyango, Ali Hassan, Alfred Ndinya, na Samuel Karanja. Watasmamia kura hizo za  kitaifa na zile za kaunti na pia kuwachagua watakaoongoza kura za mashinani. Uchaguzi hio ulismamishwa mwezi Disemba mwaka 2019 baada ya wagombeaji kukosa imani na  bodi iilyotajwa.

Wajumbe 25  kutoka shirikisho la riadha duniani IAAF, wanatarajiwa nchini wiki ijayo ili kufanya uchunguzi kabla ya Kenya kuandaa mbio za ubingwa duniani za chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20. Wajumbe hao watakagua uwanja wa Kasarni, chuo kikuu cha Kenyatta ambako wanariadha wanatarajiwa kupiga kambi, na hoteli jijini Nairobi. Rais wa shikrikisho la ridha nchini Jackson Tuwei,  anasema wajumbe hao wataongozwa na mkuu wa mawasiliano wa IAAF Jacky Brock.

Ajenti wa Gareth Bale Jonathan Barnett anasema hadhanii kama mteja wake atawahi kuregea Tottenham tena. Raia huyo wa Wales aliondoka Spurs na kuelekea Real Madrid mwaka wa 2013 kwa kitita cha pauni milioni 85 wakati huo. Kumekua na tetesi katika siku za hivi majuzi zilizomuhusisha Bale na kuregea Tottenham mwezi uliopita huku ripoti zikiashiria kwamba vilabu hivyo vilikua katika majadiliano. Barnett anasisitiza kwamba klabu hio ya North London haijawasilisha ofa yoyote kwa ajili ya Bale. Hatma ya Bale imekua ikijadiliwa sana tangu Zinedine Zidane aregee kwenye klabu hio.

Real Madrid wanapanga kuwasilisha ofa ya pauni milioni 250 kumnasa kiungo wa Paris Saint-Germain Kylian Mbappe. Mchezaji huyo wa miaka 21 raia wa Ufaransa alilumbana na meneja wa PSG Thomas Tuchel baada ya kuondolewa uwanjani wakati walipowafunga Montpellier mabao 5-0 siku ya Jumamosi. Uhusiano wa waili hao unasemekana kudorora na Mbappe huenda akaondoka.

Shirikisho la soka nchini  FKF jana lilizindua bodi itakayosimamia uchaguzi utakaofanyika Machi tarehe 30. Bodi hilo itaongozwa na Kentice Tikolo, Patrick Onyango, Ali Hassan, Alfred Ndinya, na Samuel Karanja. Watasmamia kura hizo za  kitaifa na zile za kaunti na pia kuwachagua watakaoongoza kura za mashinani. Uchaguzi hio ulismamishwa mwezi Disemba mwaka 2019 baada ya wagombeaji kukosa imani na  bodi iilyotajwa.