Mchuano kati ya Munich na Dortmund si wa kuamua bingwa wa ligi- Hansi Flick

_112433402_bayerncelebrate2019bundesligatitle
_112433402_bayerncelebrate2019bundesligatitle
Mkufunzi mkuu wa klabu ya Bayern Munich Hansi Flick amesema mchuano kati yao na mahasimu wa jadi Borrusia Dortmund si wa kuamua bingwa wa ligi hiyo.Ushindi dhidi ya Dortmund ugani Alliance Arena utaiwezesha Munich kuwa kileleni mwa ligi ya Bundesliga kwa alama saba zaidi .

 "Regardless of the result, nothing will be decided."Flick amesema.

Kwa upande wao Dortmund wana imani kuwa mlindi  Mats Hummels atakuwa tayari kushiriki kwa mechi hiyo baada ya kupata jeraha katika mechi yao ya jumamosi na amabyo walishinda magoli mawaili .

Ushindi huo uliifanya Dortmund kupunguza idadi ya alama kwa alama moja dhidi ya wapinzani wao wa jadi Munich ambao walisajili ushindi wa magoli matano .

Timu zote mbili kufikia sasa zimesajili ushindi katika mechi zao mbili baada ya ligi kurejelewa Mei 16 baada ya kusitishwa kufuatia virusi vya corona.

Bayern kwa sasa wanafukuzia taji lao la nane la Bundesliga japo litakuwa la kwanza chini ya uongozi wa Flick ambaye aliridhi mikopa kutoka kwa Niko Kovac.