Tottenham italazimika kujitolea kwa njia zote ili kubatilisha kushindwa kwao katika awamu ya kwanza ya mechi za kombe la mabingwa za 16 bora leo watakapochuana na RB Leipzig, amesema maneja Jose Mourinho.Leipzig walishinda mchuano huo wa mkondo wa kwanza bao moja kwa nunge kwa hisani ya mkwaju wa penati wa Timo Werner.Spurs walifuzu kwa fainali ya kombe hilo msimu uliopita chini ya kocha wao wa zamani Mauricio Pochettino
Valencia vs Atalanta
Valencia italenga kujaribu kubatilisha kushindwa mabao manne kwa moja dhidi ya Atalanta katika mchuano wa mkondo wa pili wa kombe la mabingwa katika uwanja wa Mestalla kwenye mechi itakayochezwa kbila mashabiki kwa ajili ya hofu ya virusi vya Corona . wenyeji watakosa huduma za mshambuliaji Maxi Gomez (jeraha la kuvunjika mguu) na mlinzi Ezequiel Garay (goti ) . Mlinzi Gabriel Paulista pia atakuwa nje ya kikosi hicho .Atalanta kwa upande wao wanatilia shaka uwezekano wa kuwepo kwa difenda wa Brazil Rafael Toloi