Allan Wanga ajiunga na Azam ya Tanzania

Picha kwa hisani ya: Twitter

Mshambulizi wa Kenya Allan Wanga  amejiunga rasmi na Azam FC ya Tanzania baada ya kutia saini mkataba wa mwaka mmoja.

Wanga ambaye alichezea AFC Leoprds, Tusker na Sofapaka amejiunga na mabingwa hao wa Tanzania kutoka Al Mereikh ya Sudan baada ya mkataba wake kukamilika.