Mwanariadha Faith Chepkoech apigwa marufuku miaka mitatu kwa matumizi ya dawa za kutitimua misuli

Mwanariadha wa Kenya Faith Chepkoech 21 awa wa hivi karibuni kuangukiwa na shoka la shirika la kupambana na ulaji muku kwa wanariadha

Muhtasari

•Mwanaridha Faith Chepkoech 21, apigwa marufuku ya miaka mitatu baada ya utumizi wa dawa za kusisimua misuli.

•Marufuku hayo yanakuja baada ya shirika amabalo linadhibiti utumiaji wa dawa za kusisimua misuli kumpata kinda huyo na kosa hilo baada ya vipimo kufanyika kwenye maabara kuu ya shirika hilo.

•Chepkoech ambaye alishinda mbio za pre-classic za mita elfu 10, atapokonywa ubingwa huo ambao alitia mfukoni kitita cha $10,000.

FAITH CHEPKOECH
Image: HISANI

Mwanariadha Faith Chepkoech mwenye umri wa miaka 21  amepigwa marufuku kushiriki mbio zozote baada ya kupatikana na hatia ya kutumia dawa za kusisimua misuli na shirika linalodhibiti utumizi wa dawa hizo. 

Katika taarifa ambayo ilitolewa na shirika hilo, Chepkoech alipatikana na hatia hiyo baada ya vipimo ambavyo vilifanyika tarehe 26 Julai,vilionyesha kuwa kinda huyo alikuwa ametumia dawa dawa aina ya EPO.

Vipimo hivyo vilichukuliwa mnamo tarehe 4 septemba  maeneo ya Iten,Elgeyo-Marakwet kutoka kwa sampuli ya mkojo kutoka kwa mwanariadha huyo na kufanyiwa vipimo kwenye maabara kuu ya shirika hilo mjini Cologne,Ujerumani.

Baada ya kupatikana kwa EPO ambayo adhabu yake ni marufuku ya miaka minne, Chepkoech alipewa kipunguzio cha mwaka mmoja baada ya kukubali kosa lake na ambalo linavunja kanuni ya 10.8.1 ya kanuni za utumizi wa dawa za kusisimua misuli.

Licha ya Chepkoech kuwa na matumaini usoni kwenye tasnia ya riadha, kwa maana atakuwa na umri wa miaka 24, wakati marufuku yake itaisha. Kutokana na marufuku hiyo Chepkoech ataupoteza ushindi wake wa riadha za pre-classic za mita elfu kumi kwa mda wa 30:22.77 ambapo alishinda kima cha $10,000.

Kufuatia kusikizwa kwa kosa lake,alipatikana kuwa hakuwa na sababu tosha za kutumia dawa hiyo na kwa hivyo kuangukiwa na shoka la marufuku ya miaka mitatu.