Straika wa Fulham Mitrovic apigwa marufuku ya mechi 8 kwa kutishia kumpiga refa

Mshambulizi huyo alipewa adhabu ya mechi 3 lakini ikaongezwa Jumanne na FA wanapanga kukata rufaa ili kuiongeza adhabu hata zaidi.

Muhtasari

• Mitrovic si wa kwanza kupokea marufuku ndefu hiyo, kwani kuna orodha ndefu ya wachezaji waliowahi kupigwa marufuku ya kushiriki mechi miezi kadhaa.

• Atarudi uwanjani kuitumikia Fulham zikiwa zimesalia mechi 2 tu kukamilika kwa msimu wa ligi kuu ya Premia.

Mshambulizi wa Fulham Aleksander Mitrovic akimsukuma refa Chris Kavanagh
Mshambulizi wa Fulham Aleksander Mitrovic akimsukuma refa Chris Kavanagh
Image: Twitter

Aleksandar Mitrovic amepewa moja ya adhabu ndefu zaidi katika historia ya Ligi ya Premia baada ya kufungiwa michezo minane kwa kumsukuma mwamuzi Chris Kavanagh katika mechi ya Fulham waliyotolewa na Manchester United kwenye Kombe la FA mwezi uliopita.

Adhabu ya kawaida ya kufungiwa mechi tatu imeongezwa hadi mechi nane, ingawa FA inapanga kukata rufaa dhidi ya adhabu hiyo, kwani wanataka mshambuliaji huyo wa Serbia apewe adhabu kubwa zaidi.

Mitrovic alitumikia mechi ya kwanza ya kufungiwa kwake katika kipigo cha 2-1 cha Fulham huko Bournemouth, na mapema zaidi anaweza kurudi ni pambano lao la Mei 13 dhidi ya Southampton - zikiwa zimesalia mechi mbili baada ya hapo.

Hata hivyo kuna matukio kumi katika historia ya Ligi Kuu ambayo yalisababisha kupigwa marufuku kwa mchezaji, sawa tu na ile Mitrovic amepokea.

Sportsmail inaangazia matukio yaliyosababisha adhabu kumi kwa muda mrefu zaidi tangu kuanzishwa kwa Ligi Kuu.

Luis Suarez (Liverpool) - michezo 8, Desemba 2011

Luis Suarez ana tofauti isiyohitajika ya kuwa mchezaji pekee kuingia kwenye orodha hii mara mbili.

Mshambulizi huyo wa Uruguay alikuwa na wakati wa kutatanisha akiwa Liverpool, na mara ya kwanza kati ya misimu miwili mirefu ya kukaa nje ya klabu hiyo ilikuja ndani ya miezi 12 baada ya kujiunga na Ajax.

Baada ya sare ya 1-1 na Manchester United mnamo Oktoba 15, 2011, Suarez alishutumiwa kwa kumtusi kwa ubaguzi wa rangi mpinzani wake Patrice Evra.

Suarez aliapa kutokuwa na hatia lakini FA baada ya kusikilizwa kwa siku saba ilimpa Suarez marufuku ya mechi nane na faini ya pauni 40,000.

Mwaka 2013 pia alipomuuma beki wa Chelsea mkono, Suarez alipewa kibano cha mechi 10 nje.

Wachezaji wa zamani Adrian Mutu wa Chelsea, Rio Ferdinand na Eric Cantona wa Man U pia wamewahi pokea marufuku ndefu Zaidi ya miezi 7, 8 na 9 mtawalia nje ya uwanja wa michezo.