Winga wa Man-U Antony aripotiwa kumpiga mrembo wake hadi kupoteza ujauzito

Kulingana na vyanz vya habari kutoka Brazil, mrembo huyo alipiga ripoti akimtuhumu Antony kwa kumpiga hadi kupoteza ujauzito wa wiki 17.

Muhtasari

• Kulingana na ripoti ya kipekee kutoka kwa jarida la Brazil, Segue a Cami, Gabriela Cavallin tayari ameomba hatua za ulinzi dhidi ya mwanasoka huyo.

• Cavalli pia alifichua kuwa haikuwa mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kumfanyia unyama.

Winga wa United akabiliwa na mashataka ya kumpiga mkewe hadi kupoteza mimba ya wiki 17.
Winga wa United akabiliwa na mashataka ya kumpiga mkewe hadi kupoteza mimba ya wiki 17.
Image: Twitter, Instagram

Winga wa Manchester United Antony yuko kwenye habari kwa mara nyingine tena, safari hii kwa sababu zisizo sahihi.

Kulingana na vyombo vya habari vya Brazil, winga huyo mwenye umri wa miaka 23 ambaye alijiunga na United kutoka Ajax msimu uliopita wa joto, ameshutumiwa kwa unyanyasaji wa nyumbani na mpenzi wake wa zamani.

Mpenzi wa zamani wa Antony, Gabriela Cavallin, aliripoti kwa polisi kwa 'unyanyasaji wa nyumbani, vitisho na majeraha ya mwili'.

Cavallin anasema Antony alimshambulia Mei 20, na ripoti hiyo inaongeza kuwa mwanamitindo huyo wa Brazil alijumuisha ‘picha za michubuko na ujumbe wa vitisho’ kutoka kwa nyota huyo wa zamani wa Ajax.

Ripoti hiyo pia inaongeza kuwa tayari imefungua uchunguzi juu ya suala hilo, hata hivyo, bado hakuna maoni yoyote rasmi yaliyotolewa na Manchester United au mchezaji huyo.

Kulingana na ripoti ya kipekee kutoka kwa jarida la Brazil, Segue a Cami, Gabriela Cavallin tayari ameomba hatua za ulinzi dhidi ya mwanasoka huyo.

Cavalli pia alifichua kuwa haikuwa mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kumfanyia unyama.

Januari mwaka huu, alisema kulitokea pambano kati ya wawili hao na Antony alimpiga, lakini aliamua kumsamehe nyota huyo wa Red Devils.

Inavyoonekana, winga huyo mwenye talanta hakuchukua uamuzi huo kwa uchangamfu.

Hata hivyo, mwezi uliopita, mrembo huyo alitangaza nia yake ya kusitisha uhusiano wao.

Habari hii inakuja huku kukiwa na masuala yanayoendelea yanayomhusu mchezaji mwingine wa Manchester United, Mason Greenwood ambaye bado amesimamishwa na klabu hiyo.

Greenwood ambaye hapo awali alishtakiwa kwa unyanyasaji wa nyumbani na unyanyasaji wa kijinsia hatimaye aliondolewa mashtaka yake mapema mwaka huu.

Hata hivyo, inabakia kuonekana nini mustakabali wa Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 21 huku kukiwa na ripoti za uhamisho kutoka Old Trafford msimu huu wa joto.