Everton wakatwa pointi 2, wiki chache baada ya kurudishiwa 4 kati ya 10 walizokatwa awali

Msururu wa madhira ambayo yanazidi kuizingira yametajwa kutokana na kukiuka Kanuni za Faida na Uendelevu za Ligi Kuu ya Uingereza.

Muhtasari

• Pigo hili linajili takribani mwezi mmoja tu baada ya kushinda rufaa waliyowasilisha baada ya kukatwa pointi 10.

• Kutokana na ushindi katika rufaa hiyo, Everton walirudishiwa point 4 baada ya hukumu kupunguzwa kutoka pointi 10 hadi 6.

Everton kupokonywa pointi
Everton kupokonywa pointi
Image: Facebook

Masaibu ya klabu ya Everton inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Premia nchini Uingereza yanaonekana kukita kambi katika lango lao baada ya kupata pigo jingine la kukatwa pointi 2 zaidi.

Pigo hili linajili takribani mwezi mmoja tu baada ya kushinda rufaa waliyowasilisha baada ya kukatwa pointi 10.

Kutokana na ushindi katika rufaa hiyo, Everton walirudishiwa point 4 baada ya hukumu kupunguzwa kutoka pointi 10 hadi 6.

 Msururu wa madhira ambayo yanazidi kuizingira yametajwa kutokana na kukiuka Kanuni za Faida na Uendelevu za Ligi Kuu ya Uingereza.

Ukiukaji huu mwingine wa mzunguko wa miaka mitatu uliomalizika msimu wa 2022/23 umewafanya kupokonywa pointi mbili na kuwaacha nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi.

Taarifa ya Ligi ya Premia inasomeka: "Tume huru imetoa punguzo la pointi mbili mara moja kwa Everton FC kwa kukiuka Kanuni za Faida na Uendelevu za Ligi ya Premia kwa kipindi kinachoishia Msimu wa 2022/23.”

"Katika kikao cha siku tatu mwezi uliopita, Tume huru ilisikiliza ushahidi na hoja kutoka kwa klabu kuhusiana na sababu mbalimbali zinazoweza kupunguza uvunjaji wake wa pauni milioni 16.6, ikiwa ni pamoja na athari za mashtaka yake mawili mfululizo ya PSR.”

“Baada ya kufanya hivyo, Tume iliamua adhabu ifaayo kuwa ni makato ya pointi mbili, na kuanza kutumika mara moja.”

"Tume huru ilithibitisha kanuni kwamba ukiukaji wowote wa PSRs ni muhimu na unahalalisha, kwa kweli unahitaji, vikwazo vya michezo."

Everton watakata rufaa dhidi ya uamuzi huo na kujibu, walisema: "Mnamo Januari 2024, Everton ilishtakiwa na Ligi Kuu kwa kukiuka vizingiti vya Faida na Uendelevu vilivyoruhusiwa kwa muda wa tathmini unaoishia 2022/23.”

“Suala hilo lilipelekwa kwa Tume ya Ligi Kuu, ambayo leo imetangaza Everton kupokea punguzo la pointi mbili mara moja.”

“Pamoja na kwamba msimamo wa Klabu ni kwamba hakuna adhabu nyingine iliyostahili, Klabu inafuraha kuona kwamba Tume imetoa sifa kwa masuala mengi yaliyoibuliwa na Klabu, ikiwamo dhana ya adhabu mara mbili, mazingira muhimu ya kupunguza Klabu kutokana na vita vya Ukraine, na kiwango cha juu cha ushirikiano na kukubali mapema uvunjaji wa Klabu.”