Cristiano Ronaldo amsifia Mbappe kama mchezaji mzuri kuliko Benzema

Benzema na Ronaldo, pamoja na Gareth Bale, waliunda timu ya utatu 'BBC' ambao ulizingatiwa sana kama moja ya wachezaji 3 wa mbele kuwahi kutokea.

Muhtasari

• Ingawa ni muhimu kutosoma sana maswali ya haraka kama haya, mchezaji huyo wa zamani wa Lyon yuko kwenye rekodi akimsifu Lionel Messi.

CR7 AMCHAGUA MBAPPE JUU YA BENZEMA
CR7 AMCHAGUA MBAPPE JUU YA BENZEMA
Image: FACEBOOK

Mwanasoka nguli duniani, Cristiano Ronaldo amezua gumzo mitandaoni kwa mara ya kwanza baada ya kukiri chaguo lake la mchezaji bora kati ya Karim Benzema na Kylian Mbappe.

Katika kipindi cha hivi majuzi kwenye chaneli yake mpya ya YouTube, UR Cristiano, mchezaji mwenzake wa zamani Rio Ferdinand alimjaribu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 kwa kumtaka Ronaldo kulinganisha safu ya wachezaji bora na baada ya kuchagua David Beckham badala ya Paul Scholes na Ryan Giggs badala ya Becks, kisha akaulizwa ni nani anayempendelea kati ya Karim Benzema na swahiba wake Kylian Mbappe.

Ronaldo bila shaka alikuwa na furaha ya kucheza pamoja na Benzema kwa miaka kadhaa wakati alipokuwa Real Madrid lakini Mbappe akiwa amewasili Bernabeu hivi majuzi, mashabiki walikuwa na hamu ya kuona nani angechaguliwa.

Hakuchukua muda kusita, Ronaldo alimsifia Mbappe, ambaye tayari amevuka jumla ya mabao ya Benzema katika kiwango cha kimataifa na 48 dhidi ya 37 ya mfungaji bora wa Al Ittihad kwa Les Bleus.

Baada ya kukaa kipindi cha mafanikio pamoja na wababe hao wa Uhispania, Benzema na Ronaldo, pamoja na Gareth Bale, waliunda timu ya utatu 'BBC' ambao ulizingatiwa sana kama moja ya wachezaji 3 wa mbele kuwahi kutokea.

Ingawa ni muhimu kutosoma sana maswali ya haraka kama haya, mchezaji huyo wa zamani wa Lyon yuko kwenye rekodi akimsifu Lionel Messi ambaye amekuwa na ushindani wa muda mrefu na nyota huyo wa Al Nassr.

Alipoulizwa mwaka 2022 kuhusu uchezaji wa Messi akiwa PSG, Benzema alimkosoa mtu yeyote ambaye anathubutu kuhoji uwezo wa mchezaji huyo wa Inter Miami.

"Messi anahitaji tu muda kuzoea," aliiambia Telefoot.

"Angalia anachofanya uwanjani, kwa vyovyote vile huwezi kumkosoa mchezaji kama huyo.

"Yeyote anayekosoa hajui lolote kuhusu soka katika uhalisia," Benzema aliendelea.