Mkusanyiko wa Habari na Matukio Muhimu Tarehe 17 Juni 2019

 

 Yaya ahukumiwa maisha jela kwa kumbala mvulana wa miaka 6 Rongo

  Yaya mmoja huko Rongo amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani kwa kumbaka na kumwambukiza  maradhi ya zinaa mtoto mvulana mwenye umri wa miaka sita . Neema Matiko  mwenye umri wa miaka 22  amepewa hukumu hiyo na  hakimu mkuu wa Rongo  Raymond Langat  kwa kosa hilo alilotekeleza machi tarehe 30 mwaka huu . Langat amesema amempa mtuhumiwa hukumu hiyo kali kwa kutumia vibaya maamaka yake kuhatarisha  maisha ya mtoto huyo licha ya kufahamu kwamba  alikuwa na maradhi ya zinaa .

Hatutaki kuwatenganisha binti zetu

 Mama za wasichana pacha kutoka kakamega  wamesema  wameshindwa jinsi ya  kuwashughulikia binti zao  baada ya  uchunguzi wa DNA kuthibitisha kwamba watoto hao ni pacha  .Rosemary Khaveleli na  Angeline Omina   hata hivyo wamesema wameamua kwamba hawatawatenganisha wasichana hao  kwani hakuna kati yao anayetaka kuishi mbali na mwenzake .

  Duka na ufamasia karibu na Hospitali ya Machakos Level Five zafungwa

Gavana wa machakos Alfred Mutua  ameongoza msako dhidi ya duka za ufamasia zinazokaribiana na  hospitali ya machakos level five   ambapo watu 12 wamekamatwa na duka hizo za dawa kufungwa . wamiliki wa duka hizo za ufamasia na maabara za kibinafsi walipewa notisi ya miezi mitatu ili kuzifunga lakini wakapuuza .

  Hakuna kisa che Ebola kilichothibitishwa 

Hatuna kisa kilichothibitishwa cha  ugonjwa wa Ebola nchini .waziri wa afya  Sicily Kariuki  amesema kundi la wataalam limemfanyia ukaguzi mgonjwa aliyelazwa huko kericho ambaye alisafiri hadi Malaba na Kuthibitisha kwamba  ugonjwa  huo hauwezi kutambuliwa kuwa Ebola . amesema kama hatua ya tahadhari sampuli kutoka kwa mgonjwa huyo imechukuliwa kufanyiwa vipimo na shirika la KEMRI .

   KWINGINEko watu watatu zaidi wametengwa katika wadi maalum  katika hospitali ya rufaa ya kericho  kufuatia kisa kimoja kinachoshukiwa kuwa cha ugonjwa wa ebola . mume wa mgonjwa aliyelazwa jana na watu wengine wawili waliomsaidia kumpeleka  mkewe hospitalini ndio waliotengw akatika wadi ingawaje hawakuwa wameonyesha daalili zinazofanana na za ugonjwa wa ebola .

 Usimwajiri mtoto -Ni hatia 

     Unajitia katika hatari ya kufungwa jela endapo utamwajiri mtoto aliye chini ya umri wa miaka 11 . wakili   Wang'oma Mola  amesema watoto aghalabu hutumiwa vibaya kwa sababu hawajui haki zao na pia mashartio ya ajira .

 Mahakama Kuu ya Eldoret yamnyima mshukiwa wa mauaji dhamana 

  Mahakama kuu huko Eldoret  imemnyima dhamana mshukiwa wa mauaji  Nafatali Kinuthia  ,aliyeshtakiwa kwa kumwua mwanafunzi wa matibabu  Ivy Wangechi . jaji Stephen Githinji amesema mshukiwa amenyimwa dhamana kwa sababu ya usalama wake  na pia kuna uwezekano atavuruga ushahidi dhidi yake endapo ataachiliwa huru .

Polisi mmoja hajapatikana tangu shambulizi la Wajir 

Afisa mmoja wa polisi hajulikani aliko  baada ya gari  lao kukanyaga bomu la kutegwa ardhini na kuwauwa maafisa saba wa polisi huko wajir  katika mpaka wa Kenya na Somalia . watatu waliokolewa wakiwa hai  ilhali mwingine aliyekuwa ametoweka alipatikana jana .

 JSC yaanza kuwaajiri majaji 11 

Tume ya huduma kwa  idara ya mahakama imeanza kuwaajiri majaji 11 wa mahakama ya rufaa ili kushughulikia upungufu uliosababishwa na  kupandishwa vyeo kwa baadhi ya majaji na wengine waliostaafu . majaji 22 na m,awakili 13  wamehojiwa kwa nafasi hizo .

Jopo la kumchunguza Jaji Jacktone Ojwang' Latajwa 

Jopo la wanachama saba limeundwa ili kuchunguza mienendo ya jaji wa mahakama ya juu zaidi Jackton Ojwang . wanachama wa jopo hilo ni pamoja na jaji mstaafu  Festus Azangalala, Ambrose Weda, Andrew Bahati Mwamuye, Lucy Kambuni, Sylvia Wanjiku Muchiri  na Amina Abda.  Jopo hilo litasimamiwa na  jaji wa mahakama ya rufaa  Alnashir Visram  na litakuwa na mawakili wawili walioteuliwa na rais Kenyatta kulisaidia katika kazi yake . vikao  vitaanza julai tarehe 15

 Ruto  huenda akapunguza Kampeini za 2022

Naibu wa rais William Ruto  huenda akaamua kupunguza kasi au akasitisha kampeini zake   kuwania urais mwaka wa 2022    baada ya rais Uhuru kenyatta kukemea vikalia wanaoendelea   kupiga siasa  . mchanganuzi wa masuala ya kisiasa Calvin Muga  hata hivyo anasem Ruto ana chaguo la kuendelea kufanya kampeini lakini nje ya chama cha Jubilee .

Waagizaji wa magari   walalamikia  Mombasa walalamikia 

  Baadhi ya waagizaji wa magari kutoka nje  huko Mombasa wanalalamikia hatua ya  serikali ya kaunti hiyo kubomoa yadi zao wanazotumia kuyauza magari hayo . wamesema serikali imepuuza agizo la mahakama lililozuia kubomolewa kwa yadi hizo  .serikali ya kaunti imedai kwamba yadi hizo zilijengwa kinyume cha sheria .

 Mwanamme ampiga mkewe kwa kumpikia wali 

Mwanamke mmoja  anauguza majeraha mabaya huko Kirinyaga baada ya kudaiwa kuchomwa na mumewe kuhusu chakula . shangazi yake mwathiriwa amesema jamaa huyo alikuwa amemtaka mkewe kumpikia  Githeri lakini badala yake mkewe akamatayarishia  wali .

Sonko na wabunge wawili waunga mkono wahudumu wa boda boda kupinga bima ya wateja

Wahudumu wa boda boda na tuk tuk  wamepata uungwaji mkono kutoka kwa gavana wa Nairobi mike sonko  na wabunge wawili katika jitiahada zao za kuzuia pendekezo la serikali kuwataka wawalipie wateja wao bima . wanataka mahakama kuzuia pendekezo hilo kwa  wakisema litaongeza gharama yao ya kufanya kazi .

 Maafisa wa Kliniki Tana River wagoma 

 Maafisa wa kliniki huko Tana River  wamegoma kulalamikia  hatua ya serikali ya kaunti  kukataa kusaini mktaba wa kuwatambua  na kushughulikia lalama zao . Katibu mkuu wa muungano wao George Gibore amesema   serikali ya kaunti ya Tana River imeyapuuza maslahi yao kwa miaka minne

Tuko tayari kukabiliana na Ebola -Waziri wa Afya 

 Waziri wa afya Sicily kariuki amewahakikishia wakenya kwamba serikali  imejitayarisha kukabiliana na ugonjwa wa Ebola .Arifa ya tahadhari kwa maafisa wote wa afya iliyotumwa na wizara ya afya ni miongoni mwa hatua zilizochukuliwa  kukabiliana na tishio la virusi hivyo.