Ni kubaya! 37% ya wakenya walishindwa kulipa kodi za nyumba mwezi Mei –utafiti

Rent
Rent
Zaidi  ya thuluthi moja ya wakenya walishindwa kulipa kodi yao ya nyumba mwezi Mei kulingana na  ripoti  ya  utafiti uliofanywa na serikali .

Ripoti hiyo inayongazia athari za kiuchumi na kijamii   za janga la corona  iliyofanywa na  shirika la takwimu nchini imesema asilimia 37 ya watu walishindwa kumudu gharama ya kodi zao mwezi Mei. Utafiti wenyewe ulifanywa mwezi Juni  na uliwahusisha watu 14,616 waliohojiwa na imefichua jinsi  virusi vya corona vilivyovuruga hali ya kiuchumi na kulemaza kipato cha watu wengi.  Kando na  kuvuruga mapato ya  watu wengi, kuna mengi ambayo watu wamejifunza wakati huu wa janga hilo kama ilivyojadiliwa kwa undani katika Podi hii  ya Yusuf Juma

&t=596s

Kulingana na utafiti huo,  takriban asilimia 30.9 ya wapangaji ambao hulipa kodi zao ndani ya muda ulioafikiwa na wenye nyumba  kabla ya janga la corona  walishindwa kulipa kodi zao mwezi Mei.

Ripoti hiyo imeonyesha kwamba  asilimia 61  ya waliokosa kulipa kodi zao walitaja kudorora kwa kipato chao kwa ajili ya janga la corona kama sababu ya kushindwa kulipa.

Mapato ya kampuni nyingi yamevurugwa kwa ajili ya janga  la corona na kuzilazimu nyingi kuwafuta kazi baadhi ya wafanyikazi.