1.Suzanna Owiyo
Mwanamuziki huyu mashuhuri wa Kenya ni mke wa pili wa Ounga Oguda kwa miaka 16 sasa. Owiyo ana mtoto moja
- Esther Passaris
Mwakilishi huyu wa akina mama Nairobi ni mke wa pili wa mfanyibiashara na mkulima mashuhuri Pius Mbugua Ngugi.
- Lilian Ng’ang’a
Lillian Ng’ang’a ni mke wa pili wa gavana wa machakos Alfred Mutua. Wawili hao hawajapata mtoto. Mutua ana mke wa kwanza Josephine Thitu Maundu.
- Mary Kilobi
Mtangazaji huyo wa KTN ni mke wa tatu wa mkuu wa COTU Francis Atwoli. Atwoli hajaficha kwamba ana wake wengi .
- Mama Ngina Kenyatta
Mama wa kwanza wa taifa alikuwa mke wa nne wa rais wa kwanza Jomo Kenyatta. Orodha ya wake za baba wa taifa ni hii.
Mke wa kwanza Grace Wahu – 1919
Mke wa pili - Edna Clarke -1942-1946
Mke wa tatu- Grace Wanjiku – 1946- 1950
Mke wan ne – Ngina Kenyatta (Mama Ngina) -1951-1978
- Sabina Chege
Mwakilishi huyu wa akina mama wa Muranga ni mke wa pili wa aliyekuwa mkuu wa bodi ya maziwa nchini Gathitu Maina.
- Jacquline Mengi
Mrembo huyo wa Tanzania na mwanamuziki alikuwa mke wa marehemu bilionea Reginald Mengi aliyeaga dunia Mei mwaka jana. Ana watoto wawili mapacha
- Cate Waruguru
Mwakilishi huyo wa akina mama wa Laikipia alikiri kuhusu ndoa yake kwa wakili William Kigen kupitia mahojiano katika runinga ya KTN. Alieleza kwamba hana soni kukiri kwamba ni mke wa pili na kwamba ana fahari sana ya kuwa na mume wake.
“ Unagundua kwamba mwanamme huyu ndiye nayetaka kuwa naye. Nataka aliye na ujasiri athubutu kunilaani kwamba nitaenda motoni kwa kuwa mke wa pili."
Aliwashauri wanawake kuelewa kwamba mwanamme ni wako tu wakati upo naye .
“ Mume wa mtu ni wake anapokuwa nyumbani. Mzee wa boma akishatoka, jitunze na uchague unachotaka katiba inaruhusu ‘ alisema Waruguru
- Yvonne Okwara
Mtangazaji huyu wa runinga ya Citizen ni mke wa pili wa Dr Andrew Matole.
Kulingana na duru, kabla ya harusi yao eneo la harusi lilibadilishwa mara kadhaa pakizuka hofu kwamba mke wa kwanza alikuwa amepanga kuikatiza harusi hiyo. Matole alikuwa na mke wa kwanza Alice Manyole ambaye wamepata watoto watatu naye.
- Emmy Kosgei
Emmy Kosgei yupo katika ndoa ya zaidi ya mke moja baada ya kushawishiwa kufunga pingu za maisha na mhubiri kutoka Nigeria Anselm Madubuko muda mfupi baada ya kukutana huko Mombasa.
Emmy na Anselm walioana mwaka wa 2013 baada ya mke wa kwanza wa raia huyo wa Nigeria Connie Uzuoamaka Madubuko kuaga dunia mwaka wa 2012.