#SemaNaRaey: Mwanadada Afurahisha Mamilioni Ya Wanaume Baada Ya Kusema Haya Kuhusu Ndoa

anita raey bleh
anita raey bleh
Katika kipindi cha Sema Na Raey ambacho huletwa kwako na mtangazaji Anita Raey, hapo ndipo uhondo wote na mafunzo ya kila aina maishani haswa kwa ndoa hupatikana.

Na kama kawaida wasikilizaji wetu ndio huwa na uhondo moto moto kwani wao ndio wenye ujuzi wa ndoa na wana ufahamu wa chenye wanandoa wafaa au hawafai kufanya.

Juzi mwanadada kwa jina Charlene aliwafurahisha mamilioni ya wanaume wa Kenya wakti alipopiga simu na kueleza jinsi mwanamke kamili anafaa kulinda na kutunza ndoa yake, haswa ikifika swala la kushughulikia mabwana zao.

"Kuishi kwa ndoa ni mambo matatu. Kitu cha kwanza ni upendo kwa nyumba, cha pili usafi na cha tatu ni kupika. Kama umeolewa kwa mfano bwanako anafanya kazi. Akitoka asubuhi unafaa kumtayarishia kila kitu na kitu unafaa kufanya ni kukutana naye kwa mlango akirudi unamjulia hali, chemshia mzee wako maji ya kuoga. Mwambie 'daddy nimepeleka maji kwa bafu'.

Kitu kingine usiwache mzee wako akae na nguo siku tatu kwani hapaswi kuvaa zaidi ya mara moja. " Aliwashauri wenzake.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be