Shujaa kukosa huduma za wachezaji watatu kutokana na majeraha

Leonard Mugaisi|Photo: .hivisasa.com

Leonard Mugaisi, Billy Odhiambo na Dennis Ombachi watakosa mikondo ya raga ya Singapore na Hong Kong kutokana na majeraha.

Watatu hao walipata majeraha hayo kwenye mashindano ya Las Vegas na Vancouver. Mugaisi alifanyiwa upasuaji siku ya jumatatu na atakua nje kwa muda wa mwezi moja.

Frank Wanyama, Nelson Oyoo na Alvin Otieno huenda wakarejeshwa kwa kikosi cha taifa kujaza nafasi zilizoachwa na watatu hao.