Timu ya raga ya 7s ya kina dada imejipatia tiketi ya kushiriki katika Olimpiki ya Tokyo Japan 2020, baada ya kufuzu katika fainali ya mashindano hayo nchini Tunisia Jumapili.
Kenya ambao ni mabingwa watetezi waliwapiga wenyeji Tunisia 19-0 kwenye michuano ya nusu finali na kujikatia tikiti ya moja kwa moja kwenda Japan
Timu hiyo ya Kenya, maarufu kama Lionesses ilikuwa timu ya nane kufuzu kwenye michezo ya Olimpiki ya 2020.
Brazil itawakilisha Amerika kusini huku Ulaya ikiwakilishwa na Uingereza ambao walifuzu katika michuano hiyo.
Ikiongozwa na kocha Felix Oloo, Lionesses walisambaratisha Zimbabwe kwa kushinda 26-5, 36-0 dhidi ya Ghana na kuwapiku Botswana Jumamosi kwa 49-0