Timu za kuangalia kwenye Europa league msimu ujao

Baada ya kumaliza shughuli zao kwenye dirisha la uhamisho,sasa ni zam zam ya klabu zilizofuzu kuwania kombe la Europa League kukabana koo.

Hata hivyo, kunazo klabu zimewasili kwenye michuano hii kwa mara ya kwanza na inatarajiwa kuwa huenda zitaleta msisimuko kwa wazee waliozoe kupiga kazi kama hii. Hata hivyo, taji hili bingwa mtetezi huwa hachezi msimu ujao.

Manchester United

Manchester united ilishindwa kutwaa tiketi ya kucheza mechi za klabu bingwa bara ulaya baada ya kumaliza ligi katika nafasi ya sita nne nyuma tatu nyuma ya Tottenham Hotspurs waliomaliza katika nafasi ya nne. Manchester United ilitajwa kuwa klabu yenye dhamana kubwa nchini Uingereza na jambo hili linaifanya kuwa timu kali kwenye michuano hii msimu uliopita.Baada ya kumaliza shughuli zao kwenye dirisha la uhamisho, sasa ni zam zam ya klabu zilizofuzu kuwania kombe la Europa League kukabana koo.

 Arsenal

Arsenali ilipoteza kwenye mchuano wa fainali wa Europa league msimu uliopita mikononi mwa Chelsea baada ya kupokea kichapo cha magoli manne kwa moja. Hata hivyo, vijana wake Unai Emery wanatarajiwa kutia fora raundi hii huku wakitarajia kushinda taji hilo.

Sevilla

Wahispaniola hawa ndio wanaongoza kwenye michuano hii kwa kushinda taji hili mara nyingi kwani wamelitwaa mara nne huku tatu kati ya hayo ikiwa ni mfululizo. Kwa sasa walimaliza katika nafasi ya tano kule nchini Uhispania hivyo wakokasa tiketi ya kucheza mechi za klabu bingwa barani ulaya. Hata hivyo, Sevilla watakumbana na ushindani mkali kutoka kwa Arsenal na Manchester United.

Wolves

 Wakali hawa kutoka ligi kuu nchini Uingereza wanatarajiwa kuja Ligi ya Europa na ubaya baada ya kuwatiwa wakali kama Chelsea tumbo joto msimu uliopita. Wolves ilimaliza katika nafasi ya saba kwenye ligi kuu nchini Uingereza huku ikiwaaacha wengi vinywa wazi. Kwa sasa Wolves imewasajili nyota kadhaa na inakisiwa kwamba wapo jioni kumtwaa kinda wa Juventus Moise Kean.

 AS Roma

As Roma ilibanduliwa katika awamu ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya msimu wa 2017/2018 na Liverpool. Roma inataraiwa kuleta upinzani wa hali ya juu pamoja na kuongeza ushindani kweye awamu ya ligi ya Europa msimu ujao hasa ikizingatiwa kwamba huenda ikamsajili mlinzi wa Totenham Hotspurs Toby ALderwield.

soma mengi hapa