Visanga vya VAR ligi kuu nchini Uingereza

Ligi kuu nchini Uingereza ilirejea wikendi iliyopita huku utumizi wa VAR ukiwa jambo lilowaacha wengi na furaha pamoja na ghadhabu vile vile.

VAR ilikuwa na matukio sabini kwa ujumla wikendi hii.

VAR inatumika kuangalia iwapo mchezaji anastahili kadi nyekundu au hafai, iwapo faulo inafaa kuwa penalti ama mchezaji mwingine alidanganya pamoja na kuyakubali magoli au kuyakataa kutokana na kuotea kwa mchezaji, kucheza vibaya na hata kunawa mpira kabla hujaingia wavuni.

 Mechi baina ya Manchester City ilishuhudia utumizi wa VAR ukiwanyima goli la pili kunako dakika ya 56 baada ya kugundulika kuwa Raheem Sterling alikuwa ameotea. Hata hivyo, VAR iliwazawadi City penalti mara ya pili baada ya mchezaji wa West Ham, Isa Diop kuonekana kukanyanga laini wakati wa upigaji wa penalti hio. Aguero alifunga penalti ya pili baada ya kuipoteza ya kwanza.

Kwenye mechi zingine, goli lake Ashley Barnes lilikataliwa na VAR baada ya kugundulika kwamba Chris wood alikuwa ameotea. Wolves kwa upande mwingine ilishuhudia goli lao limekataliwa na VAR ugani King Power Stadium baada ya Leander Dendocker kunawa mpira kabla hajacheka na wavu.

Morgan Sneiderling wa Everton alilabishwa kadi nyekundu baada ya uamuzi wa VAR kukubaliana na mwamuzi Jonathan Moss kuwa Sneiderling alistahili kadi nyekundu. Yan Valery wa Southampton aliponea kupata kadi nyekundi baada ya VAR kubadilisha uamuzi kutoka kwa referee Graham Scott aliyekuwa tayari kumtimua uwanjani dakika ya 35 baada ya kumchezea westwood kiatu.

Roberto Pereira wa Watford alinyima penalti baada ya Glen Muray wa Brighton kunawa mpira. Hata hivyo, VAR iliamua kuwa haikustahili penalti kwani ilisemekana kuwa Muray hakunawa akitaka.

VAR imeibua maswali mengi hasa kutoka na mashabiki huku kocha wa Wolves, Nuno Santos akisisitiza kuwa VAR inaharibu mchezo licha ya kuleta usawa ndani yake.