Wakili wa washatkiwa anasema kuwa mwanamke aliyenajisiwa (24) ni mtu mzima hivyo alipaswa kuwa na uwezo wa kuwazuia wawili hao kutomfanyia kitendo hicho kwani wawili hao wana umri wa miaka 23 na 22.
Hata hivyo mwanamziki huyo alisema hakuwa na uwezo wa kuzuia wawili hao.
Pamoja na hayo, mwanamziki huyo anasema kuwa hangeweza kwenda kuzungumza na polisi kwani alihofia maisha yake pamoja na kuhofia kwamba huenda asipate usaidizi kutoka na kuwa mmoja wa wawili hao ana jina 'kubwa'.
Pia, alijaribu kumweleza Wanyama baadaye kuhusu hali hio ila mchezaji huyo alifikiria kuwa mwanamziki huyo alikuwa anahitaji pesa zake. Wanyama alimfukuza na kumtaka aje na wakili kwa ajili ya suala hilo.
Awali mwaka huu mwezi julai,J aji Martha Mutuku alikuwa tayari kutoa hukumu ya wawili hao ila akasitisha kwani Mahaga hakuhudhuria koti siku hiyo kwa madai kuwa yeye ni mgonjwa.
Wakili wa mshatki ameitaka mahakama kuwafunga wawili hao kufungo cha miaka kumi na mitano ama kuwapa kifungo cha maisha gerezani.
"Ubakaji ni jambo mbaya sana. Mtu hapaswi kumtumia mwenzake vibaya kwa madai ya jinsia yake ama kwa vyovyote vile,"Wakili wake mwanamziki huyo.